Zaburi Mlango 8 Psalms

Zaburi 8:1 Psalms 8:1

Wewe, MUNGU, Bwana wetu Jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote! Wewe umeuweka utukufu wako mbinguni;

Zaburi 8:2 Psalms 8:2

Vinywani mwa watoto wachanga na wanyonyao Umeiweka misingi ya nguvu; Kwa sababu yao wanaoshindana nawe; Uwakomeshe adui na mijilipiza kisasi.

Zaburi 8:3 Psalms 8:3

Nikiziangalia mbingu zako, kazi ya vidole vyako, Mwezi na nyota ulizoziratibisha;

Zaburi 8:4 Psalms 8:4

Mtu ni kitu gani hata umkumbuke, Na binadamu hata umwangalie?

Zaburi 8:5 Psalms 8:5

Umemfanya mdogo punde kuliko Mungu; Umemvika taji ya utukufu na heshima;

Zaburi 8:6 Psalms 8:6

Umemtawaza juu ya kazi za mikono yako; Umevitia vitu vyote chini ya miguu yake.

Zaburi 8:7 Psalms 8:7

Kondoo, na ng'ombe wote pia; Naam, na wanyama wa kondeni;

Zaburi 8:8 Psalms 8:8

Ndege wa angani, na samaki wa baharini; Na kila kipitacho njia za baharini.

Zaburi 8:9 Psalms 8:9

Wewe, MUNGU, Bwana wetu, Jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote!