Zaburi Mlango 67 Psalms

Zaburi 67:1 Psalms 67:1

Mungu na atufadhili na kutubariki, Na kutuangazia uso wake.

Zaburi 67:2 Psalms 67:2

Njia yake ijulike duniani, Wokovu wake katikati ya mataifa yote.

Zaburi 67:3 Psalms 67:3

Watu na wakushukuru, Ee Mungu, Watu wote na wakushukuru.

Zaburi 67:4 Psalms 67:4

Mataifa na washangilie, Naam, waimbe kwa furaha, Maana kwa haki utawahukumu watu, Na kuwaongoza mataifa walioko duniani.

Zaburi 67:5 Psalms 67:5

Watu na wakushukuru, Ee Mungu, Watu wote na wakushukuru.

Zaburi 67:6 Psalms 67:6

Nchi imetoa mazao yake MUNGU, Mungu wetu, ametubariki.

Zaburi 67:7 Psalms 67:7

Mungu atatubariki sisi; Miisho yote ya dunia itamcha Yeye.