Zaburi Mlango 114 Psalms

Zaburi 114:1 Psalms 114:1

Haleluya. Israeli alipotoka Misri, Na Yakobo katika watu wa lugha ya kigeni.

Zaburi 114:2 Psalms 114:2

Yuda ilikuwa patakatifu pake, Israeli milki yake.

Zaburi 114:3 Psalms 114:3

Bahari iliona ikakimbia, Yordani ilirudishwa nyuma.

Zaburi 114:4 Psalms 114:4

Milima iliruka kama kondoo waume, Vilima kama wana-kondoo.

Zaburi 114:5 Psalms 114:5

Ee bahari, una nini, ukimbie? Yordani, urudi nyuma?

Zaburi 114:6 Psalms 114:6

Enyi milima, mruke kama kondoo waume? Enyi vilima, kama wana-kondoo?

Zaburi 114:7 Psalms 114:7

Tetemeka, Ee nchi, mbele za uso wa Bwana, Mbele za uso wa Mungu wa Yakobo.

Zaburi 114:8 Psalms 114:8

Augeuza mwamba kuwa ziwa la maji, Jiwe gumu kuwa chemchemi.