Zaburi Mlango 86 Psalms

Zaburi 86:1 Psalms 86:1

Ee Bwana, utege sikio lako unijibu, Maana mimi ni maskini na mhitaji

Zaburi 86:2 Psalms 86:2

Unihifadhi nafsi yangu, Maana mimi ni mcha Mungu. Wewe uliye Mungu wangu, Umwokoe mtumishi wako anayekutumaini.

Zaburi 86:3 Psalms 86:3

Wewe, Bwana, unifadhili, Maana nakulilia Wewe mchana kutwa.

Zaburi 86:4 Psalms 86:4

Uifurahishe nafsi ya mtumishi wako, Maana nafsi yangu nakuinulia Wewe, Bwana.

Zaburi 86:5 Psalms 86:5

Kwa maana Wewe, Bwana, U mwema, Umekuwa tayari kusamehe, Na mwingi wa fadhili, Kwa watu wote wakuitao.

Zaburi 86:6 Psalms 86:6

Ee Bwana, uyasikie maombi yangu; Uisikilize sauti ya dua zangu.

Zaburi 86:7 Psalms 86:7

Siku ya mateso yangu nitakuita, Kwa maana utaniitikia.

Zaburi 86:8 Psalms 86:8

Katikati ya miungu hakuna kama Wewe, Bwana, Wala matendo mfano wa matendo yako.

Zaburi 86:9 Psalms 86:9

Mataifa yote uliowafanya watakuja; Watakusujudia Wewe, Bwana, Watalitukuza jina lako;

Zaburi 86:10 Psalms 86:10

Kwa kuwa ndiwe uliye mkuu, Wewe ndiwe mfanya miujiza, Ndiwe Mungu peke yako.

Zaburi 86:11 Psalms 86:11

Ee Bwana, unifundishe njia yako; Nitakwenda katika kweli yako; Moyo wangu na ufurahi kulicha jina lako;

Zaburi 86:12 Psalms 86:12

Nitakusifu Wewe, Bwana, Mungu wangu, Kwa moyo wangu wote, Nitalitukuza jina lako milele.

Zaburi 86:13 Psalms 86:13

Maana fadhili zako kwangu ni nyingi sana; Umeiopoa nafsi yangu na kuzimu.

Zaburi 86:14 Psalms 86:14

Ee Mungu, wenye kiburi wamenishambulia; Mkutano wa wakatili wamenitafuta roho. Wala hawakukuweka Wewe Mbele ya macho yao.

Zaburi 86:15 Psalms 86:15

Lakini Wewe, Bwana, U Mungu wa rehema na neema, Mvumilivu, mwingi wa fadhili na kweli.

Zaburi 86:16 Psalms 86:16

Unielekee na kunifadhili mimi; Mpe mtumishi wako nguvu zako, Umwokoe mwana wa mjakazi wako.

Zaburi 86:17 Psalms 86:17

Unifanyie ishara ya wema, Wanichukiao waione na kuaibishwa. Kwa kuwa Wewe, Bwana, Umenisaidia na kunifariji.