Zaburi Mlango 133 Psalms

Zaburi 133:1 Psalms 133:1

Tazama, jinsi ilivyo vema, na kupendeza, Ndugu wakae pamoja, kwa umoja.

Zaburi 133:2 Psalms 133:2

Ni kama mafuta mazuri kichwani, Yashukayo ndevuni, ndevu za Haruni, Yashukayo mpaka upindo wa mavazi yake.

Zaburi 133:3 Psalms 133:3

Kama umande wa Hermoni ushukao milimani pa Sayuni. Maana ndiko Bwana alikoamuru baraka, Naam, uzima hata milele.