Zaburi Mlango 65 Psalms

Zaburi 65:1 Psalms 65:1

Ee Mungu, sifa zakulaiki katika Sayuni, Na kwako Wewe itaondolewa nadhiri.

Zaburi 65:2 Psalms 65:2

Wewe usikiaye kuomba, Wote wenye mwili watakujia.

Zaburi 65:3 Psalms 65:3

Ingawa maovu mengi yanamshinda, Wewe utayafunika maasi yetu.

Zaburi 65:4 Psalms 65:4

Heri mtu yule umchaguaye, Na kumkaribisha akae nyuani mwako. Na tushibe wema wa nyumba yako, Patakatifu pa hekalu lako.

Zaburi 65:5 Psalms 65:5

Kwa mambo ya kutisha utatujibu, Katika haki, Ee Mungu wa wokovu wetu. Wewe uliye tumaini la miisho yote ya dunia, Na la bahari iliyo mbali sana,

Zaburi 65:6 Psalms 65:6

Milima waiweka imara kwa nguvu zako, Huku ukijifunga uweza kama mshipi.

Zaburi 65:7 Psalms 65:7

Wautuliza uvumi wa bahari, Uvumi wa mawimbi yake, Na ghasia ya mataifa;

Zaburi 65:8 Psalms 65:8

Kwa hiyo wakaao mbali kabisa huogopa ishara zako; Milango ya asubuhi na jioni waifurahisha.

Zaburi 65:9 Psalms 65:9

Umeijilia nchi na kuisitawisha, Umeitajirisha sana; Mto wa Mungu umejaa maji; Wawaruzuku watu nafaka Maana ndiwe uitengenezaye ardhi.

Zaburi 65:10 Psalms 65:10

Matuta yake wayajaza maji; Wapasawazisha palipoinuka, Wailainisha nchi kwa manyunyu; Waibariki mimea yake.

Zaburi 65:11 Psalms 65:11

Umeuvika mwaka taji ya wema wako; Mapito yako yadondoza unono.

Zaburi 65:12 Psalms 65:12

Huyadondokea malisho ya nyikani, Na vilima vyajifunga furaha.

Zaburi 65:13 Psalms 65:13

Na malisho yamevikwa kondoo, Na mabonde yamepambwa nafaka, Yanashangilia, naam, yanaimba.