Zaburi Mlango 49 Psalms

Zaburi 49:1 Psalms 49:1

Sikieni haya, enyi mataifa yote; Sikilizeni, ninyi nyote mnaokaa duniani.

Zaburi 49:2 Psalms 49:2

Watu wakuu na watu wadogo wote pia, Tajiri na maskini wote pamoja.

Zaburi 49:3 Psalms 49:3

Kinywa changu kitanena hekima, Na fikira za moyo wangu zitakuwa za busara.

Zaburi 49:4 Psalms 49:4

Nitatega sikio langu nisikie mithali, Na kufumbua fumbo langu kwa kinubi

Zaburi 49:5 Psalms 49:5

Kwa nini niogope siku za uovu, Ubaya ukinizunguka miguuni pangu?

Zaburi 49:6 Psalms 49:6

Wa hao wanaozitumainia mali zao, Na kujisifia wingi wa utajiri wao;

Zaburi 49:7 Psalms 49:7

Hakuna mtu awezaye kumkomboa ndugu yake, Wala kumpa Mungu fidia kwa ajili yake,

Zaburi 49:8 Psalms 49:8

(Maana fidia ya nafsi zao ina gharama, Wala hana budi kuiacha hata milele;)

Zaburi 49:9 Psalms 49:9

ili aishi sikuzote asilione kaburi.

Zaburi 49:10 Psalms 49:10

Naam, ataliona, hata wenye hekima hufa; Mpumbavu na mjinga hupotea pamoja, Na kuwaachia wengine mali zao.

Zaburi 49:11 Psalms 49:11

Makaburi ni nyumba zao hata milele, Maskani zao vizazi hata vizazi. Hao waliotaja mashamba yao Kwa majina yao wenyewe.

Zaburi 49:12 Psalms 49:12

Lakini mwanadamu hadumu katika heshima, Bali amefanana na wanyama wapoteao.

Zaburi 49:13 Psalms 49:13

Hiyo ndiyo njia yao, ujinga wao, Nao walioko baada yao huyaridhia maneno yao.

Zaburi 49:14 Psalms 49:14

Kama kondoo wamewekwa kwenda kuzimu, Na mauti itawachunga; Watu wanyofu watawamiliki asubuhi; Umbo lao litachakaa, kao lao ni kuzimu.

Zaburi 49:15 Psalms 49:15

Bali Mungu atanikomboa nafsi yangu, Atanitoa mkononi mwa kuzimu, maana atanikaribisha.

Zaburi 49:16 Psalms 49:16

Usiogope mtu atakapopata utajiri, Na fahari ya nyumba yake itakapozidi.

Zaburi 49:17 Psalms 49:17

Maana atakapokufa hatachukua cho chote; Utukufu wake hautashuka ukimfuata.

Zaburi 49:18 Psalms 49:18

Ajapojibariki nafsi yake alipokuwa hai, Na watu watakusifu ukijitendea mema,

Zaburi 49:19 Psalms 49:19

Atakwenda kwenye kizazi cha baba zake Hawataona nuru hata milele.

Zaburi 49:20 Psalms 49:20

Mwanadamu mwenye heshima, iwapo hana akili, Amefanana na wanyama wapoteao.