Zaburi Mlango 122 Psalms

Zaburi 122:1 Psalms 122:1

Nalifurahi waliponiambia, Na twende nyumbani kwa Bwana.

Zaburi 122:2 Psalms 122:2

Miguu yetu imesimama Ndani ya malango yako, Ee Yerusalemu.

Zaburi 122:3 Psalms 122:3

Ee Yerusalemu uliyejengwa Kama mji ulioshikamana,

Zaburi 122:4 Psalms 122:4

Huko ndiko walikopanda kabila, Kabila za Bwana; Ushuhuda kwa Israeli, Walishukuru jina la Bwana.

Zaburi 122:5 Psalms 122:5

Maana huko viliwekwa viti vya hukumu, Viti vya enzi vya mbari ya Daudi.

Zaburi 122:6 Psalms 122:6

Utakieni Yerusalemu amani; Na wafanikiwe wakupendao;

Zaburi 122:7 Psalms 122:7

Amani na ikae ndani ya kuta zako, Na kufanikiwa ndani ya majumba yako.

Zaburi 122:8 Psalms 122:8

Kwa ajili ya ndugu zangu na rafiki zangu Niseme sasa, Amani ikae nawe.

Zaburi 122:9 Psalms 122:9

Kwa ajili ya nyumba ya Bwana, Mungu wetu, Nikutafutie mema.