Zaburi Mlango 136 Psalms
Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
Mshukuruni Mungu wa miungu; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
Mshukuruni Bwana wa mabwana; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
Yeye peke yake afanya maajabu makuu; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
Yeye aliyefanya mbingu kwa fahamu zake; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
Yeye aliyeitandaza nchi juu ya maji; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
Yeye aliyefanya mianga mikubwa; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
Jua litawale mchana; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
Mwezi na nyota zitawale usiku; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
Yeye aliyewapiga Wamisri kwa kuwaua wazaliwa wa kwanza wao; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
Akawatoa Waisraeli katikati yao; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
Kwa mkono hodari na mkono ulionyoshwa; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
Yeye aliyeigawa Bahari ya Shamu; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
Akawavusha Israeli katikati yake; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
Akamwangusha Farao na jeshi lake katika Bahari ya Shamu; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
Yeye aliyewaongoza watu wake jangwani; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
Yeye aliyewapiga wafalme wakuu; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
Akawaua wafalme mashuhuri; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
Sihoni, mfalme wa Waamori; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
Na Ogu, mfalme wa Bashani; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
Akaitoa nchi yao iwe urithi; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
Urithi wa Israeli mtumishi wake; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
Aliyetukumbuka katika unyonge wetu; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
Akatuokoa na watesi wetu; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
Kila chenye mwili akipa chakula chake; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
Mshukuruni Mungu wa mbingu; Kwa maana fadhili zake ni za milele.