Zaburi Mlango 11 Psalms

Zaburi 11:1 Psalms 11:1

Bwana ndiye niliyemkimbilia. Mbona mnaiambia nafsi yangu, Kimbia kama ndege mlimani kwenu?

Zaburi 11:2 Psalms 11:2

Maana, tazama, wasio haki wanaupinda uta, Wanaitia mishale yao katika upote, Ili kuwapiga gizani wanyofu wa moyo.

Zaburi 11:3 Psalms 11:3

Kama misingi ikiharibika, Mwenye haki atafanya nini?

Zaburi 11:4 Psalms 11:4

Bwana yu katika hekalu lake takatifu. Bwana ambaye kiti chake kiko mbinguni, Macho yake yanaangalia; Kope zake zinawajaribu wanadamu.

Zaburi 11:5 Psalms 11:5

Bwana humjaribu mwenye haki; Bali nafsi yake humchukia asiye haki, Na mwenye kupenda udhalimu.

Zaburi 11:6 Psalms 11:6

Awanyeshee wasio haki mitego, Moto na kiberiti na upepo wa hari, Na viwe fungu la kikombe chao.

Zaburi 11:7 Psalms 11:7

Kwa kuwa Bwana ndiye mwenye haki, Apenda matendo ya haki, Wanyofu wa moyo watamwona uso wake.