Zaburi Mlango 131 Psalms

Zaburi 131:1 Psalms 131:1

Bwana, moyo wangu hauna kiburi, Wala macho yangu hayainuki. Wala sijishughulishi na mambo makuu, Wala na mambo yashindayo nguvu zangu.

Zaburi 131:2 Psalms 131:2

Hakika nimeituliza nafsi yangu, Na kuinyamazisha. Kama mtoto aliyeachishwa Kifuani mwa mama yake; Kama mtoto aliyeachishwa, Ndivyo roho yangu ilivyo kwangu.

Zaburi 131:3 Psalms 131:3

Ee Israeli, umtarajie Bwana, Tangu leo na hata milele.