Zaburi Mlango 112 Psalms

Zaburi 112:1 Psalms 112:1

Haleluya. Heri mtu yule amchaye Bwana, Apendezwaye sana na maagizo yake.

Zaburi 112:2 Psalms 112:2

Wazao wake watakuwa hodari duniani; Kizazi cha wenye adili kitabarikiwa.

Zaburi 112:3 Psalms 112:3

Nyumbani mwake mna utajiri na mali, Na haki yake yakaa milele.

Zaburi 112:4 Psalms 112:4

Nuru huwazukia wenye adili gizani; Ana fadhili na huruma na haki.

Zaburi 112:5 Psalms 112:5

Heri atendaye fadhili na kukopesha; Atengenezaye mambo yake kwa haki.

Zaburi 112:6 Psalms 112:6

Kwa maana hataondoshwa kamwe; Mwenye haki atakumbukwa milele.

Zaburi 112:7 Psalms 112:7

Hataogopa habari mbaya; Moyo wake u imara ukimtumaini Bwana.

Zaburi 112:8 Psalms 112:8

Moyo wake umethibitika hataogopa, Hata awaone watesi wake wameshindwa.

Zaburi 112:9 Psalms 112:9

Amekirimu, na kuwapa maskini, Haki yake yakaa milele, Pembe yake itatukuzwa kwa utukufu.

Zaburi 112:10 Psalms 112:10

Asiye haki ataona na kusikitika, Atasaga meno yake na kuyeyuka, Tamaa ya wasio haki itapotea.