Zaburi Mlango 150 Psalms

Zaburi 150:1 Psalms 150:1

Haleluya. Msifuni Mungu katika patakatifu pake; Msifuni katika anga la uweza wake.

Zaburi 150:2 Psalms 150:2

Msifuni kwa matendo yake makuu; Msifuni kwa kadiri ya wingi wa ukuu wake.

Zaburi 150:3 Psalms 150:3

Msifuni kwa mvumo wa baragumu; Msifuni kwa kinanda na kinubi;

Zaburi 150:4 Psalms 150:4

Msifuni kwa matari na kucheza; Msifuni kwa zeze na filimbi;

Zaburi 150:5 Psalms 150:5

Msifuni kwa matoazi yaliayo; Msifuni kwa matoazi yavumayo sana.

Zaburi 150:6 Psalms 150:6

Kila mwenye pumzi na amsifu Bwana. Haleluya.