Zaburi Mlango 56 Psalms

Zaburi 56:1 Psalms 56:1

Mungu, unirehemu, maana yuko atakaye kunimeza, Mchana kutwa ananionea akileta vita.

Zaburi 56:2 Psalms 56:2

Adui zangu wanataka kunimeza mchana kutwa, Maana waletao vita juu yangu kwa kiburi ni wengi.

Zaburi 56:3 Psalms 56:3

Siku ya hofu yangu nitakutumaini Wewe;

Zaburi 56:4 Psalms 56:4

Kwa msaada wa MUNGU nitalisifu neno lake. Nimemtumaini Mungu, sitaogopa; Mwenye mwili atanitenda nini?

Zaburi 56:5 Psalms 56:5

Mchana kutwa wanapotosha maneno yangu, Mawazo yao yote ni juu yangu kunitakia mabaya.

Zaburi 56:6 Psalms 56:6

Hukutanika, hujificha, huziangalia nyayo zangu, Kwa kuwa wameniotea nafsi yangu.

Zaburi 56:7 Psalms 56:7

Je! Wataokoka kwa uovu wao? Ee Mungu, uwaangamize kwa hasira yako.

Zaburi 56:8 Psalms 56:8

Umehesabu kutanga-tanga kwangu; Uyatie machozi yangu katika chupa yako; (Je! Hayamo katika kitabu chako?)

Zaburi 56:9 Psalms 56:9

Ndipo adui zangu watarudi nyuma siku ile niitapo. Neno hili najua kuwa MUNGU yu upande wangu;

Zaburi 56:10 Psalms 56:10

Kwa msaada wa MUNGU nitalisifu neno lake. Kwa msaada wa Bwana nitalisifu neno lake.

Zaburi 56:11 Psalms 56:11

Nimemtumaini Mungu, sitaogopa; Mwanadamu atanitenda nini?

Zaburi 56:12 Psalms 56:12

Ee Mungu, nadhiri zako zi juu yangu; Nitakutolea dhabihu za kushukuru.

Zaburi 56:13 Psalms 56:13

Maana umeniponya nafsi yangu na mauti; Je! Hukuizuia miguu yangu isianguke? Ili nienende mbele za Mungu Katika nuru ya walio hai.