Zaburi Mlango 146 Psalms

Zaburi 146:1 Psalms 146:1

Haleluya. Ee nafsi yangu, umsifu Bwana.

Zaburi 146:2 Psalms 146:2

Nitamsifu Bwana muda ninaoishi, Nitamwimbia Mungu wangu ningali ni hai.

Zaburi 146:3 Psalms 146:3

Msiwatumainie wakuu, Wala binadamu ambaye hakuna wokovu kwake.

Zaburi 146:4 Psalms 146:4

Pumzi yake hutoka, huurudia udongo wake, Siku hiyo mawazo yake yapotea.

Zaburi 146:5 Psalms 146:5

Heri ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake, Na tumaini lake ni kwa Bwana, Mungu wake,

Zaburi 146:6 Psalms 146:6

Aliyezifanya mbingu na nchi, Bahari na vitu vyote vilivyomo. Huishika kweli milele,

Zaburi 146:7 Psalms 146:7

Huwafanyia hukumu walioonewa, Huwapa wenye njaa chakula; Bwana hufungua waliofungwa;

Zaburi 146:8 Psalms 146:8

Bwana huwafumbua macho waliopofuka; Bwana huwainua walioinama; Bwana huwapenda wenye haki;

Zaburi 146:9 Psalms 146:9

Bwana huwahifadhi wageni; Huwategemeza yatima na mjane; Bali njia ya wasio haki huipotosha.

Zaburi 146:10 Psalms 146:10

Bwana atamiliki milele, Mungu wako, Ee Sayuni, kizazi hata kizazi. Haleluya.