Zaburi Mlango 121 Psalms

Zaburi 121:1 Psalms 121:1

Nitayainua macho yangu niitazame milima, Msaada wangu utatoka wapi?

Zaburi 121:2 Psalms 121:2

Msaada wangu u katika Bwana, Aliyezifanya mbingu na nchi.

Zaburi 121:3 Psalms 121:3

Asiuache mguu wako usogezwe; Asisinzie akulindaye;

Zaburi 121:4 Psalms 121:4

Naam, hatasinzia wala hatalala usingizi, Yeye aliye mlinzi wa Israeli.

Zaburi 121:5 Psalms 121:5

Bwana ndiye mlinzi wako; Bwana ni uvuli mkono wako wa kuume.

Zaburi 121:6 Psalms 121:6

Jua halitakupiga mchana, Wala mwezi wakati wa usiku.

Zaburi 121:7 Psalms 121:7

Bwana atakulinda na mabaya yote, Atakulinda nafsi yako.

Zaburi 121:8 Psalms 121:8

Bwana atakulinda utokapo na uingiapo, Tangu sasa na hata milele.