Zaburi Mlango 30 Psalms

Zaburi 30:1 Psalms 30:1

Ee Bwana, nitakutukuza kwa maana umeniinua, Wala hukuwafurahisha adui zangu juu yangu.

Zaburi 30:2 Psalms 30:2

Ee Bwana, Mungu wangu, Nalikulilia ukaniponya.

Zaburi 30:3 Psalms 30:3

Umeniinua nafsi yangu, Ee Bwana, kutoka kuzimu. Umenihuisha na kunitoa Miongoni mwao washukao shimoni.

Zaburi 30:4 Psalms 30:4

Mwimbieni Bwana zaburi, Enyi watauwa wake. Na kufanya shukrani. Kwa kumbukumbu la utakatifu wake.

Zaburi 30:5 Psalms 30:5

Maana ghadhabu zake ni za kitambo kidogo, Katika radhi yake mna uhai. Huenda kilio huja kukaa usiku, Lakini asubuhi huwa furaha.

Zaburi 30:6 Psalms 30:6

Nami nilipofanikiwa nalisema, Sitaondoshwa milele.

Zaburi 30:7 Psalms 30:7

Bwana, kwa radhi yako Wewe uliuimarisha mlima wangu. Uliuficha uso wako, Nami nikafadhaika.

Zaburi 30:8 Psalms 30:8

Ee Bwana, nalikulilia Wewe, Naam, kwa Bwana naliomba dua.

Zaburi 30:9 Psalms 30:9

Mna faida gani katika damu yangu Nishukapo shimoni? Mavumbi yatakusifu? Yataitangaza kweli yako?

Zaburi 30:10 Psalms 30:10

Ee Bwana, usikie, unirehemu, Bwana, uwe msaidizi wangu.

Zaburi 30:11 Psalms 30:11

Uligeuza matanga yangu kuwa machezo; Ulinivua gunia, ukanivika furaha.

Zaburi 30:12 Psalms 30:12

Ili utukufu wangu ukusifu, Wala usinyamaze. Ee Bwana, Mungu wangu, Nitakushukuru milele.