Zaburi Mlango 58 Psalms

Zaburi 58:1 Psalms 58:1

Ni kweli, enyi wakuu, mnanena haki? Enyi wanadamu, mnahukumu kwa adili?

Zaburi 58:2 Psalms 58:2

Sivyo! Mioyoni mwenu mnatenda maovu; Katika nchi mnapima udhalimu wa mikono yenu.

Zaburi 58:3 Psalms 58:3

Wasio haki wamejitenga tangu kuzaliwa kwao; Tangu tumboni wamepotea, wakisema uongo.

Zaburi 58:4 Psalms 58:4

Sumu yao, mfano wake ni sumu ya nyoka; Mfano wao ni fira kiziwi azibaye sikio lake.

Zaburi 58:5 Psalms 58:5

Asiyeisikiliza sauti ya waganga, Ijapo wanafanya uganga kwa ustadi.

Zaburi 58:6 Psalms 58:6

Ee Mungu, uyavunje meno yao vinywani mwao; Ee Bwana, uyavunje magego ya wana-simba.

Zaburi 58:7 Psalms 58:7

Na watoweke kama maji yapitayo kwa kasi; Akiielekeza mishale yake, iwe imetiwa ubutu.

Zaburi 58:8 Psalms 58:8

Kama konokono ayeyukaye na kutoweka, Kama mimba iliyoharibika, isiyoliona jua,

Zaburi 58:9 Psalms 58:9

Kabla ya masufuria yenu kupata moto wa miiba, Ataipeperusha kama chamchela, Iliyo mibichi na iliyo moto.

Zaburi 58:10 Psalms 58:10

Mwenye haki atafurahi akionapo kisasi; Ataiosha miguu yake katika damu ya wasio haki.

Zaburi 58:11 Psalms 58:11

Na mwanadamu atasema, Hakika iko thawabu yake mwenye haki. Hakika yuko Mungu Anayehukumu katika dunia.