Zaburi Mlango 70 Psalms

Zaburi 70:1 Psalms 70:1

Ee Mungu, uniokoe, Ee Bwana, unisaidie hima.

Zaburi 70:2 Psalms 70:2

Waaibike, wafedheheke, Wanaoitafuta nafsi yangu. Warudishwe nyuma, watahayarishwe, Wapendezwao na shari yangu.

Zaburi 70:3 Psalms 70:3

Warudi nyuma, na iwe aibu yao, Wanaosema, Ewe! Ewe!

Zaburi 70:4 Psalms 70:4

Washangilie, wakufurahie, Wote wakutafutao. Waupendao wokovu wako Waseme daima, Atukuzwe Mungu.

Zaburi 70:5 Psalms 70:5

Nami ni maskini na mhitaji, Ee Mungu, unijilie kwa haraka. Ndiwe msaada wangu na mwokozi wangu, Ee Bwana, usikawie.