Zaburi Mlango 138 Psalms

Zaburi 138:1 Psalms 138:1

Nitakushukuru kwa moyo wangu wote, Mbele ya miungu nitakuimbia zaburi.

Zaburi 138:2 Psalms 138:2

Nitasujudu nikilikabili hekalu lako takatifu, Nitalishukuru jina lako, Kwa ajili ya fadhili zako na uaminifu wako, Kwa maana umeikuza ahadi yako, Kuliko jina lako lote.

Zaburi 138:3 Psalms 138:3

Siku ile niliyokuita uliniitikia, Ukanifariji nafsi kwa kunitia nguvu.

Zaburi 138:4 Psalms 138:4

Ee Bwana, wafalme wote wa dunia watakushukuru, Watakapoyasikia maneno ya kinywa chako.

Zaburi 138:5 Psalms 138:5

Naam, wataziimba njia za Bwana, Kwa maana utukufu wa Bwana ni mkuu.

Zaburi 138:6 Psalms 138:6

Ingawa Bwana yuko juu, amwona mnyenyekevu, Naye amjua mwenye kujivuna tokea mbali.

Zaburi 138:7 Psalms 138:7

Nijapokwenda kati ya shida utanihuisha, Utanyosha mkono juu ya hasira ya adui zangu, Na mkono wako wa kuume utaniokoa.

Zaburi 138:8 Psalms 138:8

Bwana atanitimilizia mambo yangu; Ee Bwana, fadhili zako ni za milele; Usiziache kazi za mikono yako.