Zaburi Mlango 4 Psalms

Zaburi 4:1 Psalms 4:1

Ee Mungu wa haki yangu, uniitikie niitapo; Umenifanyizia nafasi wakati wa shida; Unifadhili na kuisikia sala yangu.

Zaburi 4:2 Psalms 4:2

Enyi wanadamu, hata lini utukufu wangu utafedheheka? Je! Mtapenda ubatili na kutafuta uongo?

Zaburi 4:3 Psalms 4:3

Bali jueni ya kuwa Bwana amejiteulia mtauwa; Bwana atasikia nimwitapo.

Zaburi 4:4 Psalms 4:4

Mwe na hofu wala msitende dhambi, Tafakarini vitandani mwenu na kutulia.

Zaburi 4:5 Psalms 4:5

Toeni dhabihu za haki, Na kumtumaini Bwana.

Zaburi 4:6 Psalms 4:6

Wengi husema, Nani atakayetuonyesha mema? Bwana, utuinulie nuru ya uso wako.

Zaburi 4:7 Psalms 4:7

Umenitia furaha moyoni mwangu, Kupita yao wanapozidishiwa nafaka na divai.

Zaburi 4:8 Psalms 4:8

Katika amani nitajilaza na kupata usingizi mara, Maana Wewe, Bwana, peke yako, Ndiwe unijaliaye kukaa salama.