Zaburi Mlango 113 Psalms

Zaburi 113:1 Psalms 113:1

Haleluya. Enyi watumishi wa Bwana, sifuni, Lisifuni jina la Bwana.

Zaburi 113:2 Psalms 113:2

Jina la Bwana lihimidiwe Tangu leo na hata milele.

Zaburi 113:3 Psalms 113:3

Toka maawio ya jua hata machweo yake Jina la Bwana husifiwa.

Zaburi 113:4 Psalms 113:4

Bwana ni mkuu juu ya mataifa yote, Na utukufu wake ni juu ya mbingu.

Zaburi 113:5 Psalms 113:5

Ni nani aliye mfano wa Bwana, Mungu wetu aketiye juu;

Zaburi 113:6 Psalms 113:6

Anyenyekeaye kutazama, Mbinguni na duniani?

Zaburi 113:7 Psalms 113:7

Humwinua mnyonge kutoka mavumbini, Na kumpandisha maskini kutoka jaani.

Zaburi 113:8 Psalms 113:8

Amketishe pamoja na wakuu, Pamoja na wakuu wa watu wake.

Zaburi 113:9 Psalms 113:9

Huweka nyumbani mwanamke aliye tasa, Awe mama ya watoto mwenye furaha.