Zaburi Mlango 126 Psalms

Zaburi 126:1 Psalms 126:1

Bwana alipowarejeza mateka wa Sayuni, Tulikuwa kama waotao ndoto.

Zaburi 126:2 Psalms 126:2

Ndipo kinywa chetu kilipojaa kicheko, Na ulimi wetu kelele za furaha. Ndipo waliposema katika mataifa, Bwana amewatendea mambo makuu.

Zaburi 126:3 Psalms 126:3

Bwana alitutendea mambo makuu, Tulikuwa tukifurahi.

Zaburi 126:4 Psalms 126:4

Ee Bwana, uwarejeze watu wetu waliofungwa, Kama vijito vya Kusini.

Zaburi 126:5 Psalms 126:5

Wapandao kwa machozi Watavuna kwa kelele za furaha.

Zaburi 126:6 Psalms 126:6

Ingawa mtu anakwenda zake akilia, Azichukuapo mbegu za kupanda. Hakika atarudi kwa kelele za furaha, Aichukuapo miganda yake.