Zaburi Mlango 149 Psalms

Zaburi 149:1 Psalms 149:1

Haleluya. Mwimbieni Bwana wimbo mpya, Sifa zake katika kusanyiko la watauwa.

Zaburi 149:2 Psalms 149:2

Israeli na amfurahie Yeye aliyemfanya, Wana wa Sayuni na wamshangilie mfalme wao.

Zaburi 149:3 Psalms 149:3

Na walisifu jina lake kwa kucheza, Kwa matari na kinubi wamwimbie.

Zaburi 149:4 Psalms 149:4

Kwa kuwa Bwana awaridhia watu wake, Huwapamba wenye upole kwa wokovu.

Zaburi 149:5 Psalms 149:5

Watauwa na waushangilie utukufu, Waimbe kwa sauti kuu vitandani mwao.

Zaburi 149:6 Psalms 149:6

Sifa kuu za Mungu na ziwe vinywani mwao, Na upanga mkali kuwili mikononi mwao.

Zaburi 149:7 Psalms 149:7

Ili kufanya kisasi juu ya mataifa, Na adhabu juu ya kabila za watu.

Zaburi 149:8 Psalms 149:8

Wawafunge wafalme wao kwa minyororo, Na wakuu wao kwa pingu za chuma.

Zaburi 149:9 Psalms 149:9

Kuwafanyia hukumu iliyoandikwa; Hiyo ndiyo heshima ya watauwa wake wote. Haleluya.