Zaburi Mlango 52 Psalms

Zaburi 52:1 Psalms 52:1

Kwa nini kujisifia uovu, Ewe jabari? Wema wa Mungu upo sikuzote.

Zaburi 52:2 Psalms 52:2

Ulimi wako watunga madhara, Kama wembe mkali, Ewe mwenye hila

Zaburi 52:3 Psalms 52:3

Umependa mabaya kuliko mema, Na uongo kuliko kusema kweli.

Zaburi 52:4 Psalms 52:4

Umependa maneno yote ya kupoteza watu, Ewe ulimi wenye hila.

Zaburi 52:5 Psalms 52:5

Lakini Mungu atakuharibu hata milele; Atakuondolea mbali; Atakunyakua hemani mwako; Atakung'oa katika nchi ya walio hai.

Zaburi 52:6 Psalms 52:6

Nao wenye haki wataona; Wataingiwa na hofu na kumcheka;

Zaburi 52:7 Psalms 52:7

Kumbe! Huyu ndiye mtu yule, Asiyemfanya Mungu kuwa nguvu zake. Aliutumainia wingi wa mali zake, Na kujifanya hodari kwa madhara yake.

Zaburi 52:8 Psalms 52:8

Bali mimi ni kama mzeituni Umeao katika nyumba ya Mungu. Nazitumainia fadhili za Mungu milele na milele.

Zaburi 52:9 Psalms 52:9

Nitakushukuru milele kwa maana umetenda; Nitalingojea jina lako kwa kuwa ni jema; Mbele ya wacha Mungu wako.