Zaburi Mlango 75 Psalms

Zaburi 75:1 Psalms 75:1

Ee Mungu, twakushukuru. Twakushukuru kwa kuwa Jina lako li karibu; Watu huyasimulia matendo yako ya ajabu.

Zaburi 75:2 Psalms 75:2

Nitakapoufikia wakati ulioamriwa, Mimi nitahukumu hukumu za haki.

Zaburi 75:3 Psalms 75:3

Ingawa dunia na wote wakaao humo wataharuki, Mimi mwenyewe nimezisimamisha nguzo zake.

Zaburi 75:4 Psalms 75:4

Naliwaambia waliojivuna, Msijivune; Na wasio haki, Msiiinue pembe.

Zaburi 75:5 Psalms 75:5

Msiiinue pembe yenu juu, Wala msinene kwa shingo ya kiburi.

Zaburi 75:6 Psalms 75:6

Maana siko mashariki wala magharibi, Wala nyikani itokako heshima.

Zaburi 75:7 Psalms 75:7

Bali Mungu ndiye ahukumuye; Humdhili huyu na kumwinua huyu.

Zaburi 75:8 Psalms 75:8

Maana mkononi mwa Bwana mna kikombe, Na mvinyo yake inatoka povu; Kumejaa machanganyiko; Naye huyamimina. Na sira zake wasio haki wa dunia Watazifyonza na kuzinywa.

Zaburi 75:9 Psalms 75:9

Bali mimi nitatangaza matendo yako milele, Nitamwimbia Mungu wa Yakobo.

Zaburi 75:10 Psalms 75:10

Pembe zote za wasio haki nitazikata, Na pembe za mwenye haki zitainuka.