Zaburi Mlango 47 Psalms

Zaburi 47:1 Psalms 47:1

Enyi watu wote, pigeni makofi, Mpigieni Mungu kelele kwa Sauti ya shangwe.

Zaburi 47:2 Psalms 47:2

Kwa kuwa Bwana Aliye juu, mwenye kuogofya, Ndiye mfalme mkuu juu ya dunia yote.

Zaburi 47:3 Psalms 47:3

Atawatiisha watu wa nchi chini yetu, Na mataifa chini ya miguu yetu.

Zaburi 47:4 Psalms 47:4

Atatuchagulia urithi wetu, Fahari ya Yakobo ambaye alimpenda.

Zaburi 47:5 Psalms 47:5

Mungu amepaa kwa kelele za shangwe, Bwana kwa sauti ya baragumu.

Zaburi 47:6 Psalms 47:6

Mwimbieni Mungu, naam, imbeni; Mwimbieni mfalme wetu, naam, imbeni.

Zaburi 47:7 Psalms 47:7

Maana Mungu ndiye mfalme wa dunia yote, Imbeni kwa akili.

Zaburi 47:8 Psalms 47:8

Mungu awamiliki mataifa, Mungu ameketi katika kiti chake kitakatifu.

Zaburi 47:9 Psalms 47:9

Wakuu wa watu wamekusanyika, Wawe watu wa Mungu wa Ibrahimu. Maana ngao za dunia zina Mungu, Ametukuka sana.