Zaburi Mlango 129 Psalms

Zaburi 129:1 Psalms 129:1

Mara nyingi wamenitesa tangu ujana wangu, Israeli na aseme sasa,

Zaburi 129:2 Psalms 129:2

Mara nyingi wamenitesa tangu ujana wangu, Lakini hawakuniweza.

Zaburi 129:3 Psalms 129:3

Wakulima wamelima mgongoni mwangu, Wamefanya mirefu mifuo yao.

Zaburi 129:4 Psalms 129:4

Bwana ndiye mwenye haki, Amezikata kamba zao wasio haki.

Zaburi 129:5 Psalms 129:5

Na waaibishwe, warudishwe nyuma, Wote wanaoichukia Sayuni.

Zaburi 129:6 Psalms 129:6

Na wawe kama majani ya darini Yanyaukayo kabla hayajamea.

Zaburi 129:7 Psalms 129:7

Ambayo mvunaji haujazi mkono wake, Wala mfunga miganda kifua chake.

Zaburi 129:8 Psalms 129:8

Wala hawasemi wapitao, Amani ya Bwana ikae nanyi, Twawabariki kwa jina la Bwana.