Zaburi Mlango 128 Psalms

Zaburi 128:1 Psalms 128:1

Heri kila mtu amchaye Bwana, Aendaye katika njia yake.

Zaburi 128:2 Psalms 128:2

Taabu ya mikono yako hakika utaila; Utakuwa heri, na kwako kwema.

Zaburi 128:3 Psalms 128:3

Mkeo atakuwa kama mzabibu uzaao, Vyumbani mwa nyumba yako. Wanao kama miche ya mizeituni Wakiizunguka meza yako.

Zaburi 128:4 Psalms 128:4

Tazama, atabarikiwa hivyo, yule amchaye Bwana.

Zaburi 128:5 Psalms 128:5

Bwana akubariki toka Sayuni; Uone uheri wa Yerusalemu siku zote za maisha yako;

Zaburi 128:6 Psalms 128:6

Naam, ukawaone wana wa wanao. Amani ikae na Israeli.