Zaburi Mlango 127 Psalms

Zaburi 127:1 Psalms 127:1

Bwana asipoijenga nyumba Waijengao wafanya kazi bure. Bwana asipoulinda mji Yeye aulindaye akesha bure.

Zaburi 127:2 Psalms 127:2

Kazi yenu ni bure, mnaoamka mapema, Na kukawia kwenda kulala, Na kula chakula cha taabu; Yeye humpa mpenzi wake usingizi.

Zaburi 127:3 Psalms 127:3

Tazama, wana ndio urithi wa Bwana, Uzao wa tumbo ni thawabu.

Zaburi 127:4 Psalms 127:4

Kama mishale mkononi mwa shujaa, Ndivyo walivyo wana wa ujanani.

Zaburi 127:5 Psalms 127:5

Heri mtu yule Aliyelijaza podo lake hivyo. Naam, hawataona aibu Wanaposema na adui langoni.