Zaburi Mlango 142 Psalms

Zaburi 142:1 Psalms 142:1

Kwa sauti yangu nitamlilia Bwana, Kwa sauti yangu nitamwomba Bwana dua.

Zaburi 142:2 Psalms 142:2

Nitafunua mbele zake malalamiko yangu, Shida yangu nitaitangaza mbele zake.

Zaburi 142:3 Psalms 142:3

Nilipozimia roho uliyajua mapito yangu; Katika njia niendayo wamenifichia mtego.

Zaburi 142:4 Psalms 142:4

Utazame mkono wa kuume ukaone, Kwa maana sina mtu anijuaye. Makimbilio yamenipotea, Hakuna wa kunitunza roho.

Zaburi 142:5 Psalms 142:5

Bwana, nimekuita nikasema, Ndiwe kimbilio langu, Fungu langu katika nchi ya walio hai.

Zaburi 142:6 Psalms 142:6

Ukisikilize kilio changu, Kwa maana nimedhilika sana. Uniponye nao wanaonifuatia, Kwa maana wao ni hodari kuliko mimi.

Zaburi 142:7 Psalms 142:7

Uitoe nafsi yangu kifungoni. Nipate kulishukuru jina lako. Wenye haki watanizunguka, Kwa kuwa Wewe unanikirimu.