Zaburi Mlango 125 Psalms

Zaburi 125:1 Psalms 125:1

Wamtumainio Bwana ni kama mlima Sayuni, Ambao hautatikisika, wakaa milele.

Zaburi 125:2 Psalms 125:2

Kama milima inavyouzunguka Yerusalemu, Ndivyo Bwana anavyowazunguka watu wake, Tangu sasa na hata milele.

Zaburi 125:3 Psalms 125:3

Kwa maana fimbo ya udhalimu Haitakaa juu ya fungu la wenye haki; Wenye haki wasije wakainyosha Mikono yao kwenye upotovu.

Zaburi 125:4 Psalms 125:4

Ee Bwana, uwatendee mema walio wema, Nao walio wanyofu wa moyo.

Zaburi 125:5 Psalms 125:5

Bali wao wanaozigeukia njia zao zilizopotoka, Bwana atawaondoa pamoja na watenda maovu. Amani ikae na Israeli.