Zaburi Mlango 98 Psalms

Zaburi 98:1 Psalms 98:1

Mwimbieni Bwana wimbo mpya, Kwa maana ametenda mambo ya ajabu. Mkono wa kuume wake mwenyewe, Mkono wake mtakatifu umemtendea wokovu.

Zaburi 98:2 Psalms 98:2

Bwana ameufunua wokovu wake, Machoni pa mataifa ameidhihirisha haki yake.

Zaburi 98:3 Psalms 98:3

Amezikumbuka rehema zake, Na uaminifu wake kwa nyumba ya Israeli. Miisho yote ya dunia imeuona Wokovu wa Mungu wetu.

Zaburi 98:4 Psalms 98:4

Mshangilieni Bwana, nchi yote, Inueni sauti, imbeni kwa furaha, imbeni zaburi.

Zaburi 98:5 Psalms 98:5

Mwimbieni Bwana zaburi kwa kinubi, Kwa kinubi na sauti ya zaburi.

Zaburi 98:6 Psalms 98:6

Kwa panda na sauti ya baragumu. Shangilieni mbele za Mfalme, Bwana.

Zaburi 98:7 Psalms 98:7

Bahari na ivume na vyote viijazavyo, Ulimwengu nao wanaokaa ndani yake.

Zaburi 98:8 Psalms 98:8

Mito na ipige makofi, Milima na iimbe pamoja kwa furaha.

Zaburi 98:9 Psalms 98:9

Mbele za Bwana; Kwa maana anakuja aihukumu nchi. Atauhukumu ulimwengu kwa haki, Na mataifa kwa adili.