Zaburi Mlango 64 Psalms

Zaburi 64:1 Psalms 64:1

Mungu, uisikie sauti yangu katika malalamiko yangu; Unilinde uhai wangu na hofu ya adui.

Zaburi 64:2 Psalms 64:2

Utanificha mbali na shauri la siri la watenda mabaya, Mbali na ghasia ya watu wafanyao maovu;

Zaburi 64:3 Psalms 64:3

Waliounoa ulimi wao kama upanga, Wameielekeza mishale yao, maneno ya uchungu,

Zaburi 64:4 Psalms 64:4

Wapate kumpiga mkamilifu faraghani, Kwa ghafula humpiga wala hawaogopi.

Zaburi 64:5 Psalms 64:5

Walijifanya hodari katika jambo baya; Hushauriana juu ya kutega mitego; Husema, Ni nani atakayeiona?

Zaburi 64:6 Psalms 64:6

Hutunga maovu; husema, Tumefanya shauri kamili; Na mawazo ya ndani ya kila mmoja wao, Na moyo wake, huwa siri kabisa.

Zaburi 64:7 Psalms 64:7

Kwa hiyo Mungu atawapiga shabaha, Kwa mshale mara watapigwa.

Zaburi 64:8 Psalms 64:8

Ndivyo watakavyokwazwa, Ulimi wao wenyewe ukishindana nao. Wote wawaonao watatikisa kichwa.

Zaburi 64:9 Psalms 64:9

Na watu wote wataogopa, Wataitangaza kazi ya Mungu, Na kuyafahamu matendo yake.

Zaburi 64:10 Psalms 64:10

Mwenye haki atamfurahia Bwana na kumkimbilia, Na wote wenye moyo wa adili watajisifu.