Zaburi Mlango 63 Psalms

Zaburi 63:1 Psalms 63:1

Ee MUNGU, Mungu wangu, nitakutafuta mapema, Nafsi yangu inakuonea kiu, Mwili wangu wakuonea shauku, Katika nchi kame na uchovu, isiyo na maji.

Zaburi 63:2 Psalms 63:2

Ndivyo nilivyokutazama katika patakatifu, Nizione nguvu zako na utukufu wako.

Zaburi 63:3 Psalms 63:3

Maana fadhili zako ni njema kuliko uhai; Midomo yangu itakusifu.

Zaburi 63:4 Psalms 63:4

Ndivyo nitakavyokubariki maadamu ni hai; Kwa jina lako nitaiinua mikono yangu.

Zaburi 63:5 Psalms 63:5

Nafsi yangu itakinai kama kushiba mafuta na vinono; Kinywa changu kitakusifu kwa midomo ya furaha.

Zaburi 63:6 Psalms 63:6

Ninapokukumbuka kitandani mwangu, Nakutafakari Wewe makesha yote ya usiku.

Zaburi 63:7 Psalms 63:7

Maana Wewe umekuwa msaada wangu, Na uvulini mwa mbawa zako nitashangilia.

Zaburi 63:8 Psalms 63:8

Nafsi yangu inakuandama sana; Mkono wako wa kuume unanitegemeza.

Zaburi 63:9 Psalms 63:9

Bali waitafutao nafsi yangu, ili kuiharibu, Wataingia pande za nchi zilizo chini.

Zaburi 63:10 Psalms 63:10

Watatolewa wafe kwa nguvu za upanga, Watakuwa riziki za mbwa-mwitu.

Zaburi 63:11 Psalms 63:11

Bali mfalme atamfurahia Mungu, Kila aapaye kwa Yeye atashangilia, Kwa maana vinywa vya waongo vitafumbwa.