Zaburi Mlango 6 Psalms

Zaburi 6:1 Psalms 6:1

Bwana, usinikemee kwa hasira yako, Wala usinirudi kwa ghadhabu yako.

Zaburi 6:2 Psalms 6:2

Bwana, unifadhili, maana ninanyauka; Bwana, uniponye, mifupa yangu imefadhaika.

Zaburi 6:3 Psalms 6:3

Na nafsi yangu imefadhaika sana; Na Wewe, Bwana, hata lini?

Zaburi 6:4 Psalms 6:4

Bwana urudi, uniopoe nafsi yangu, Uniokoe kwa ajili ya fadhili zako.

Zaburi 6:5 Psalms 6:5

Maana mautini hapana kumbukumbu lako; Katika kuzimu ni nani atakayekushukuru?

Zaburi 6:6 Psalms 6:6

Nimechoka kwa kuugua kwangu; Kila usiku nakieleza kitanda changu; Nalilowesha godoro langu kwa machozi yangu.

Zaburi 6:7 Psalms 6:7

Jicho langu limeharibika kwa masumbufu, Na kuchakaa kwa sababu yao wanaoniudhi.

Zaburi 6:8 Psalms 6:8

Ondokeni kwangu, ninyi nyote mtendao uovu; Kwa kuwa Bwana ameisikia sauti ya kilio changu.

Zaburi 6:9 Psalms 6:9

Bwana ameisikia dua yangu; Bwana atayatakabali maombi yangu.

Zaburi 6:10 Psalms 6:10

Adui zangu wote wataaibika na kufadhaika, Watarudi nyuma, kwa ghafula wataaibika.