Zaburi Mlango 23 Psalms

Zaburi 23:1 Psalms 23:1

Bwana ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu.

Zaburi 23:2 Psalms 23:2

Katika malisho ya majani mabichi hunilaza, Kando ya maji ya utulivu huniongoza.

Zaburi 23:3 Psalms 23:3

Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.

Zaburi 23:4 Psalms 23:4

Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji.

Zaburi 23:5 Psalms 23:5

Waandaa meza mbele yangu, Machoni pa watesi wangu. Umenipaka mafuta kichwani pangu, Na kikombe changu kinafurika.

Zaburi 23:6 Psalms 23:6

Hakika wema na fadhili zitanifuata Siku zote za maisha yangu; Nami nitakaa nyumbani mwa Bwana milele.